Siri ya misingi ya upendo wa kweli
MWL. MICHAEL L. KIHWELE
Zaburi 18:32-33” Mungu ndiye anijaliaye
nguvu kila upande; ndiye anayeifanya salama njia yangu. Ameiimaraisha miguu yangu
kama ya paa, na kuniweka salama juu ya vilele.
Naomba Watanzania wenzangu na Afrika Mashariki pamoja Africa nzima na dunia yote kwa lugha zote mnisaidie kutangaza habari hii ili tupone. Let us talk in one voice to make the world peace and love.
Naomba Watanzania wenzangu na Afrika Mashariki pamoja Africa nzima na dunia yote kwa lugha zote mnisaidie kutangaza habari hii ili tupone. Let us talk in one voice to make the world peace and love.
Biblia
inasema nini?
Neno
la mwisho ni hili, muwe na nia moja,
wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitivu, wanyenyekevu, watu
wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu
hiyo ndiyo mlioitiwa ili mrithi Baraka. 1 Petro 3:8-9
Maana
kwa jinsi Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanae wa pekee afe msalabani
ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele. Yohana 3:6
Zaburi 19:7 “Sheria ya Bwana ni kamilifu,
humpa mtu uhai mpya; shuhuda za Bwana ni za kweli, huwapa hekima wasio na
makuu.
Yohana16:6
“Yesu akamwambia, mimi ndimi njia ya kweli na uzima, mtu hawezi kwenda kwa baba
bila kupitia kwangu”
Waebrania 13: 1 “Upendo
wa ndugu na uzidi kudumu msisahau kuwafadhiri wageni maana kwa njia kama hii
wengi wamewapokea malaika pasipo kujua
Shukrani
Awali ya yote namshukuru Mungu muumba wa
mbingu na dunia pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Pili nawashukuru wazazi
wangu kwa kukubali kunilea katika maadili ambayo hata hivi leo nasubutu
kuandika kitabu hiki: hizi zote ni matunda ya malezi yao. Tatu napenda
kutanguliza shukrani zangu za dhati ziende kwa Bw. Emmanuel Lucas Kihwele
ambaye ni kaka yangu wa kwanza pia ndiye mlezi wangu kielimu niliyo nayo
pengine sikustahili kuipata, ni jitihada zake. Naomba Mungu ambariki yeye na
mke wake. Pia namshukuru mke wangu kipenzi Magreth Mathias Nkwabi, kwa usikivu
na uvumilivu alionao katika kufanikisha uandishi wa kitabu hiki.
Nitakuwa
mchoyo wa shukrani kama nitamwacha nyuma rafiki yangu wa damu, Mwl Salehe Amiri
Mtamike na mke wake Witness Mussa Nakembetwa kwa ushirikiano na upendo
walionionesha pindi naandika kitabu hiki na maisha ya kila siku tunaishi
kiujumla; naomba Mungu azidi kudumisha ushirikiano wetu
Mwisho
kabisa napenda kurudisha shukrani zangu za pekee kwa ndugu yangu Mch. Madson
Lukas Kihwele kwa kunifundisha upendo pale ninapokata tamaa. Pia ndugu zangu
wote Nawapongeza kwa kunifundisha mwenendo mzuri wenye maadili ya Kiafrika,
Mungu mwenyezi awabariki wote.
Nini
maana ya upendo?
Upendo ni msukumo
wa asili ,ambao hatuwezi kuulazimisha
kuwa nao, lakinini kila mmoja anahitaji kuwa nao au ahitaji kupoteza hisia
zake. Japokuwa watu wengi wanaamini kuwa upendo ni ufahamu ambao kimiujiza
humfanya mtu kuonekana yuko sawa na watu wengi kumwamini na kutokuwa na mashaka
naye.
Kulingana na
historia ya wanafalsafa mbalimbali duniani, tangu miaka 400 iliyopita ya
historia ya kitaalamu duniani,kama ilivyo nakiliwa na mwanafalsafa Maria Popova
“Upendo hauna kitu chochote cha kufanya juu
ya kile
Utarajiacho kupata -ila tu katika yale
utarajiayo
Kutoa - ambayo ni kila kitu.”
Upendo hauangalii
mema mangapi umetendewa, bali mazuri mangapi umeyatenda au unatarajia kutenda
katika jamii yako, ukizingatia hayo moyoni mwako,utaamsha hisia ya upendo na
huruma nafsini mwako katika kujali na kusaidia maisha ya watu wengine pamoja na
kulinda haki za watu na kuheshimu thamani zao.
Kwahiyo upendo
unaweza kumbadilisha mtu kama vile mzazi awezavyo kubadili mwenendo wa mwanae.
Hakuna mahusiano ya kibinadamu katika jamii yoyote ile duniani isipokuwa kwa
njia ya upendo.
Kwa hiyo watu
wawili au zaidi wanapotofautiana kauli, hisia au mtazamo huwapelekea kutokuelewana,
na matokeo ya kutokuelewana ni chuki, husuda, kiburi, hasira na visasi na
upendo kutoweka. Hari hii inaweza kuanza baina ya mtu na mtu, familiya na
familiya, koo moja na koo nyingine, pahala pa kazi, chama kimoja na chama
kingine cha siasa, au nchi moja na nchi nyingine zilizopishana kisiasa. Upendo
ukitoweka hauna mbadala yake, Upendo ukitawala katika jamii yoyote duniani
huleta amani baina ya wanajamii.
Shakespeare katika
simulizi lake lenye jina la “A mid summer
Night’s Dream”:
Ameeleza kuwa
“Upendo hauonekani kwa macho, bali nafsini
kwa mtu”.
Kumbe upendo
huanza moyoni mwa mtu, na kisha huambatana na matendo yake ya nje pamoja na
kauli. Kwasababu kimtokacho mtu ndivyo alivyo nafsini mwake. Ukisoma katika
kitabu kiatakatifu Biblia:
Mithali 23: 7a- Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo
Kwani upendo
hauhesabu makosa, haujivuni, hautakabali bali huvumilia. Lakini roho isiyo na
upendo haina uvumilivu, imejawa na kiburi, kisasi, husuda, hasira na ubinafsi.
Bila kusahau majivuno na kujiinua.
Nini
chanzo cha Upendo?
Chanzo cha upendo
alionao mtu ni kazi kuuelezea, kutegemeana na mtazamo wa mtu na jinsi alivyo
moyoni mwake, pia namna ya moyo wa mtu unavyoridhika katika kutendewa, kutenda
na kuthaminiwa na jamii anayoishi nayo. Kwasababu kila mtu anaweza kueleza
chanzo cha upendo kulingana na hisia zake zilizo moyoni mwake. Mtu aliye na
hisia za mapenzi huweza kusema upendo
chanzo chake ni kumjali mwenzi wako, au kutimiza ndoto za mwenzi wako kulingana
na makubaliano yao. Aidha kwa watu walio na hisia za
maendeleo, huweza kusema kuwa upendo chanzo chake ni kutokuwa na husuda na tamaa
mbaya kwa maendeleo ya mtu mwingine. Kujali na kuheshimu maisha ya watu wengine
bila kujali tofauti za kiuchumi, kisiasa na kidini.
Lakini mwanafalsafa
mmoja, James Baldwin (1948- 1985) katika simulizi lenye jina la “The
Price of the Ticket”. Amesema
kama ifuatavyo juu ya upendo
“Upendo hauna mwanzo wala mwisho kwa namna
tunavyo
fikili ulivyo, lakini upendo ni kupambana,
upendo ni vita.
Upendo unakuwa kadiri mtu akuavyo.”
Hivyo basi upendo
ni tabia ambayo mtu amezaliwa nayo, na kisha kadiri akuavyo na upendo ulio
moyoni mwake ukuwa na kutoa matunda yake. Mtu aliye na upendo moyoni mwake kila
wakati huwa na furaha na kila mtu, hahesabii makosa ni mwenye roho ya kusamehe,
asiyekumbuka mabaya na mwenye kuhesabia jema moja kwa mabaya mia moja,
mvumilivu, hasiye na haraka katika kutenda kwa msukumo wa hasira. Mtu hasiye
mbinafsi wa haki na hasiye na dharau katika mambo madogo yanayowapata watu
wengine, hususani matatizo ya kiafya, kiuchumi na kielimu, kwasababu kwa asili
yake hakuna tatizo lilo dogo na kufurahiwa.,
Louis
de Bazac-
amesema hivi
“Kadiri
mtu ahukumuvyo, ndivyo kadiri upendo upunguavyo”
Upendo ni vigumu
sana kuuelewa, lakini ni zaidi ya jinsi ujuavyo asili ya kitu Fulani.
Ukimfikiria mtu katika mambo mabaya wakati wote hakika hautampenda. Jaribu sana
kumfikiria mtu katika mtazamo chanya, hali hii mara zote inaimarisha umoja wa
watu walio na utamaduni mmoja na utaratibu wa jamii moja, unaongozwa na kanuni
moja ya maisha.
Je, upendo huleta haki?
Mtu akiwa na
upendo yuko radhi kafa kwa ajili ya mtu mwema, lakini kwa mwanadamu wa sasa
hakuna hata mtu mmoja ambaye yuko tayari kufa kwa ajili ya mwenye haki. Ndiyo
kwanza wenye haki wanafungwa, wananyongwa na kuumizwa hata kufa kwa sababu
upendo umegeuzwa kwa kutegemea kitu apokeacho mtu. Madhara ya upendo wa namana
hiyo kumezaa rushwa na ufisadi. Ukisoma katika biblia takatifu katika kitabu
cha Warumi 5:7 utaona kuwa mwanadamu
ni mtu wa kujipenda mwenyewe. Huthamini sana vya kwake na nafsi yake kuliko
nafsi ya mwingine. Hayuko mtu aliyetayari kutetea haki ya mtu mwingine, kila
mtu huona kuwa ana haki kuliko mwingine hata kama hakustahili haki. Na ndiyo
maana watu wanawaua wenzao kwa ajili ya kuzitosheleza nafsi zao. Ona mauaji ya
vikongwe kule Shinyanga Tanzania, ona mauaji ya maalubino kwa ajili ya kupata
utajiri, yote hii ni kwa sababu ya kutothamini haki za watu wengine za kuishi
duniani. Majambazi nao hupora na kuua watu kwa ajili ya kujipenda wenyewe,
wanasiasa mbalimbali huanzisha mapigano kwa kutumia silaha nzito kwa ajili ya
kutimiza haja ya nafsi zao za kuwa viongozi bila kuthamini maisha ya watu
wengine. Kumbe haki hutafutwa kwa njia ya mazungumzo.
Warumi
5:7- “Kwakuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu
mwenye haki”,
lakini yawezekana mtu
kuthubutu kufa
kwa ajili ya mtu aliye mwema.
Upendo wa namna
hii tunauita ni upendo wa kiungwana,uliozaidi ya kibinadamu. Yaani ni upendo wa
Mungu mwenyewe ambao katika Yesu kristo
tumepokea upatanisho wa mioyo yetu, ambao kwa ajili yetu kristo alikufa
ili sisi tuliokuwa adui wenye dhambi tupatanishwe na Mungu kwa njia ya mauti yake. Huu ni upendo upitao fadhiri za
kibinadamu, kwa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya uhai wa watu wengine wakosaji wenye dhambi.
Warumi
5:8 - Bali Mungu aonesha pendo lake yeye
mwenyewe kwetu
sisi, kristo alikufa kwa ajili
yetu
tulipokuwa tungali wenye dhambi.
Mtu akiwa na
upendo moyoni ni jambo jema. Hatakubali mwenye haki aonewe, atafanya kila
linalowezekana kumnusuru mwenye haki. Kama mama ahangaikiavyo kumnusuru mwanae pindi
awapo mgonjwa au mwenye njaa kwa kuwa mama ni mtu mwenye upendo sana kwa
mwanae. Japo baadhi ya wanawake wanawaua wana wao mara baada ya kuwazaa, au
kuwatupa porini au majalalani kwa sababu ya ugumu wa maisha au matatizo ya
kifamilia ambayo huwapelekea katika mfadhaiko wa mawazo na kisha kupelekea
mjengeko wa roho za kikatili badala ya upendo moyoni mwao. Lakini kovu la matendo kama hayo hayafutiki mpaka mwisho
wa uhai wao, kwa sababu walivyoumbwa ni kuwa na upendo.
Laiti kama wanaume tungaliimarisha upendo
kwa dada, mama na wake zetu, watoto wa mitaani wasingalikuwepo, wala mauaji ya
kikatili duniani yangepungua. Kwa sababu vitokeapo vita wanaotaabika sana ni
wanawake na watoto, kwanini? Kwa sababu mama hayuko tayari kukimbia kuwaacha
watoto wake, wanaune wanawatenda vibaya wanawake na watoto wasio na hatia. Kwa
kuwa upendo haupo ndani yao. Mimi ni mwafrika, naweza kuthubutu kusema jamii ya
kiafrika tumepungukiwa na upendo au hatuna upendo kabisa, kwasababu bara zima
la Afrika tunaangalia watu wachache wenye roho zisizo na upendo kuwafanyia
ukatili watu wengi wasio na hatia kuangamia. Pengine baadhi ya nchi kupeleka
majeshi yao kupora mali na kuwasaidia wenye roho za ukatili kuua wengine pasipo
kujali. Japo kuna baadhi ya nchi barani Afrika zilizo mstari wa mbele kusaidia
kurudisha mshikamano baina ya nchi
zilizo na vita, kwa mfano;Tanzania, Uganda Kenya na Rwanda hizi ni baadhi ya
nchi chache za Afrika zilizo kifua mbele kuwahurumia waafrika wengine kwa
kupeleka majeshi yao kulinda amani. Japo zingine zipo pia za namna hiyohiyo
Afrika.
Biblia takatifu
inatuonya katika katabu kile cha waraka wa Paulo
mtume kwa Wathesalonike wa pili
3:11-15
“Maana twasikia kwamba wako watu
kwenu waendao bila utaratibu,hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha
na mambo ya wengine. Basi twaagiza hao, na kuwaonya katika Bwana Yesu
Kristo,watende kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe. Lakini ninyi
ndugu msikate tamaa katika kutenda mema. Lakini ikiwa mtu awaye yote hashiriki neno
letu la waraka huu, jihadharinini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate
kutahayari: Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.”
Wanadamu! Mungu
wetu aketiye mahali pa juu sana ametuumba tuishi katika hali ya utaratibu,
kufanya kazi kwa bidii, uvumilivu, kuonyana na upendo. Utaratibu huu wa
kufuatilia mambo na kufanya kazi za watu wengine kwa manufaa yao na siasa za
kiuchumi wa chi zao na kuoneana, huo sio utaratibu utokao kwa Mungu Yule aliye
tuumba bali unatoka kwa miungu ya kishetani ambao ndani yake kumejaa uharibifu
mkubwa.
Ni fursa nyingine
kwa watu wa Afrika kukataa kata kata fursa ya vita kama suluhu ya matatizo
yetu, badala yake tujikite katika sera na mikakati inayopania kujenga na
kudumisha misingi ya haki, amani, upendo na upatanisho wa kweli kati ya watu.
Maisha ni zawadi kutoka kwa mwenyezi Mungu, yanapaswa kulindwa tangu pale mtoto
anapotungwa mimba tumboni mwa mama yake. ( kauli ya baraza la maaskofu katoliki
Afrika)
Mtume Paulo katika
waraka wake wa kwanza kwa Timotheo, amasema
” Wala wasianagalie hadithi na nasaba zisizo
na ukomo, ziletazo maswali wala si madaraka ya Mungu yaliyo katika imani; basi
ufanye hivyo. Walakini mwisho wa agizo hilo ni upendo utokao katika moyo safi
na dhamira njema, na imani isiyo na unafiki. Wengine wakiyakosa hayo wamegeukia
maneno ya ubatili; Wapenda kuwa waalimu wa sheria, ingawa hawayafahamu wasemayo
wala mambo yale wayanenaye kwa uthabiti.” 1Timotheo 1:4-6
Kutokana na maneno
hayo matakatifu kama yalivyo nenwa na mtume Paulo kwa Timotheo. Kiongozi lazima
awe na upendo utokao katika moyo safi na dhamira njema. Watu waliokosa upendo
na moyo safi hugeukia katika ukatili, mauaji, utekaji nyara, uchawi na uvunjaji
wa sheria, yaani kupotosha hukumu. Asiwepo katika pahala fulani kiongozi hasiye
na dhamira njema, kama akiwepo lazima pahara pale amani ikosekane.
Amani ikikosekana
katika jamii yoyote ile duniani, upendo hutoweka na upendo ukitoweka katika
jamii,basi jamii hiyo haitatawalika.
Biblia inaendelea
kutufundisha kwa kusema kwamba
“Lakini
twajua ya kuwa sheria ni njema,
kama mtu akiitumia kwa njia iliyo
halali” (1 Timotheo 1:8)
Unapokuwa kiongozi
au msimamizi wa sheria, Vitabu vitakatifu tunavyoviamini sisi waamini wa dini
mbalimbali duniani vinatufundisha kuwa; watu waasi, wasio wataratibu sheria na
iwabane. Usiruhusu watu kudhurumu haki ya watu wema. Usiseme uongo wala usiibe
mali ya umma. Hivyo vyote ni ishara ya kutokuwa na upendo, usipende pesa mbele
kabla ya haki, ukifanya hivyo unaruhusu mianya ya rushwa. Na mianya ya rushwa
ikitawala itawagawa watu unaowaongoza, kutakuwa na tabaka la watu wenye kipato
na tabaka la wanyonge wasio na kipato cha kutoa kitu chochote ili wasikilizwe
na kutatuliwa kelo na shida zao.
Matokeo ya hayo
yote watu watakosa uzalendo na nchi yao,
viongozi wao, vyombo vya sheria na haki, pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama
na kujenga chuki na serikali yao. Chuki ikitawala amani hutoweka, na amani ikitoweka
upendo nao hudhoofika mioyoni mwa watu, hatima ya yote mapigano ya wenyewe kwa
wenyewe, maandamano na migomo katika taasisi za serikali na kwa jamii
unayoitawala kwa ujumla, pamoja na ubabaishaji mwingi katika utoaji wa huduma
za kijamii.
Raisi wa awamu ya
nne katika utawala wa Tanzania baada ya uhuru Dr. Jakaya M. Kikwete, amewahi kusema katika moja ya hotuba yake
redioni (mwaka 2014) kwamba:
“ Amani na upendo vikitoweka havina mbadala
yake
isipokuwa mafarakano na mauaji”
Kiongozi mzuri ni
Yule anayelinda na kusimamia vizuri katiba ya jamii yake, kwa kuwa katiba ni
makubaliano ya wengi yaliyofanywa kwa mahojiano ya pamoja yanayotambulika
kisheria.
Wanasheria wahukumu
kwa haki kwa kulinda amani na upendo wa nchi yao. Kadhalika na askari nao
walinde rasrimali na uhuru wa watu walio katika nchi yao.
Na wewe ulioajiriwa unatakiwa kuwa na upendo
wa kuhudumia wengine na kuridhika katika kile unachopata, kwani kumbuka kuna
wengine hawana hicho unachopata wewe, japo wanaishi katika jamii unayoishi wewe
na wanahaki sawa kama wewe, lakini hutegemea shughuli zao za kila siku. Mtu
yeyote akikosa kuzingatia hayo basi huyo amekosa upendo, kwani upendo
huimarisha uwajibikaji katika yale utarajiayo kuyatenda.
Je
Upendo huleta viongozi bora?
Ninyi ni kama
wanadamu vijana, watoto na wazee wa urithi ulio nadra, ni watoto halisi wa
Mungu mmezaliwa katika nyakati hizi maalumu za kihistoria ya dunia kwa kusudi
takatifu la Mungu. Wakati na zama hizi za sasa maadili ya kitabia na kidini ya
jamii yanaonekana kudhoofika katika jamii nyingi duniani kote. Aidha mabadiliko
na maendeleo ya kisiasa yanaendelea kupamba moto, pia mageuzi ya kisayansi na
tekenolojia yamekuwa makubwa pasipo kifani. Dunia imefanywa kuwa kama kijiji,
hivyo na ufahamu wa watu umeongezeka. Hivyo basi dunia imekuwa pahala pasipo
tawalika kiurahisi. Kiongozi yeyote wa zama hizi za utandawazi aanatakiwa kuwa
na upendo, elimu na maarifa pamoja na maadili mema.
Biblia inasema:
“Angalieni
nimemweka kuwa shahidi kwa kabila za watu;
kuwa kiongozi na jemadari kwa kabila za watu” (Isaya 55:4)
Kumbe uongozi
umewekwa na Mungu mwenyezi, huotoa mwongozo wenye nguvu ya kutatua matatizo ya
jamii kwa mafanikio. Ukiona kiongozi yeyote duniani antoa mwongozo wenye
kuwadhuru watu anaowaongoza basi ujue amepungukiwa na upendo au pengine hana
upendo kabisa.
Katika kitabu ch
Warumi 12:7-10, Biblia inaelezea kwamba:
“Ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu;
mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake. Mwenye kuonya, katika kuonya kwake;
mwenye kukarimu kwa moyo mweupe, mwenye kusimamia kwabidii mwenye kurehemu, kwa
furaha. Pendo na lisiwe na unafiki, lichukieni lililo ovu, mkiambatana na
lililo jema”.
Kiongozi bora ni
yule mwenye uwezo wa kutumia mamlaka aliyonayo vizuri, katika kukemea, kuonya
na kutoa maamuzi sahihi yasiyoweza kufukuza amani bali yenye kuimarisha
mshikamano, amani na upendo miongoni mwa watu anaowaongoza. Ni mtu mwenye
kulinda kauli ya midomo yake na hasiye mwepesi katika kunena bali aliye
mvumilivu mwenye moyo safi usio na unafiki, mpenda haki na mwaminifu.
Wanafalsafa
mbalimbali duniani wa uongozi, wanasema kiongozi bora anaweza kuleta mabadiliko
na mageuzi ya utendaji katika mfumo wa kiutendaji wa utoaji wa huduma ya jamii,
hivyo kiongozi bora anpaswa kuwa na huruma kwa wafanyakazi wanaotoa huduma kwa
jamii, ili watumishi hao wawe na upendo na kazi zao, kisha kuongoza bidii
katika kazi zao kwa moyo. Viongozi wanapaswa kutenda kama vile wangependa
wafuasi wao watende, kwa kufanya hivo watakuwa wamegusa tafsiri ya neno upendo.
Upendo
huokoa Taifa bali Amani huinua uchumi wa Taifa
Watu wakiwa na
upendo pahala popote duniani au taifa lolote lile ulimwenguni, Taifa hilo huwa
na amani. Na amani ikiwepo basi katika pahala hapo huwa na maendeleo ya kidemokrasia
na uchumi. Mimi kama Mtanzania mzawa naona hamasa sana kuishawishi jamii ya
Kitanzania kuulinda mshikamano tulionao ambao tumepewa kama dhamana ya upendo
tulionao, ambao kwa sasa umetufanya tudumu katika umoja tulionao na kutuwezesha
katika mshikamano tunaodumu nao hata hivi leo, ulioletwa na waasisi wetu wawili
ambao ni hayati Mwl. J.K Nyerere pamoja na A.A Karume. Hili ni jambo la
kupokelewa kwa mikono miwili na kulienzi. Mshikamano ni chanzo cha umoja wetu
na uzalendo wa Watanzania, nawashawishi vijana wa Kitanzania kuwa na uzalendo
wa nchi yetu. Tusikubali kuwa madaraja na ngazi katika kulididimiza taifa letu
wenyewe. Uchumi wa nchi hii utaletwa na kuinuliwa kwa umoja na uzalendo wa Watanzania
wote, bila kujali wewe ni nani, unaelimu gani? Unacheo gani? Umesomea kada
gani? Muumini wa dini gani au unatoka katika kabila lipi. Tukisimama katika
muungano wa umoja wetu, hayupo wa kutugombanisha, umoja ni silaha kubwa ya
ushindi wenye tija kwa maendeleo ya kila Mtanzania. Tuthamini rasrimali za
taifa letu Tanzania, tuwaheshimu waliotutangulia kiumri, tuwe wasikivu tunapoelimishwa
na watu waliokuwa mbele yetu kidesturi, elimu hisiwe kama silaha ya kukwamisha
maendeleo ya shughuli za kijamii.
Wasomi wawe mstari
wa mbele katika kuisaidia jamii kutatua migogoro itokanayo na mabadiliko ya
kitekinolojia, siasa na kiuchumi duniani. Kwasababu ni lahisi kwa wasomi kujua
wapi tuliko toka, tulipo na tunako kwenda, tusipuuze, tuwe na upendo wa ustawi
wa taifa letu. Ukombozi wa taifa hili umo mikononi mwa Watanzania wote, tusipodumisha amani na upendo tutakuwa
wakimbizi katika taifa letu. Hii ni kauli ya mama Maria J.K Nyerere katika moja ya hotuba zake redioni.
Watanzania
tunamengi ya kujifunza kutoka kwa aliyekuwa waziri Mkuu wa tatu wa Tanzania,
hayati Edward Moringe Sokoine kwa jinsi alivyokuwa kielelezo cha kupigania
wanyonge (Waziri Mkuu Mizengo Pinda amenena kauli
hiyo siku ya Jumanne, Aprili, 12, 2011).” Marehemu
Sokoine atakumbukwa kwa mengi ambayo tukiyaongelea hatutaweza kuyamaliza, tunamkumbuka
mtu ambaye kwetu sisi Watanzania ni kielelezo bora cha utumishi, kujituma,
upendo na kupenda haki na kielelezo cha kumcha na kumtumikia Mungu.
Askofu
wa jimbo katoliki Dodoma, Mhashamu Askofu Gervas John Nyaisonga katika moja ya
ibada zake, alisema kumbukumbu ya kifo cha Sokoine kiwakumbushe Watanzania ni
nini cha kujifunza kutoka kwake katika kuenzi tunu alizoacha. Alisema alikuwa
mtu wa kipekee kwani alijitolea kukatwa 50% ya mshahara wake ili kuchangia
katika mfuko wa nguvu kazi ili wananchi wasio na uwezo wa kukopa benki waweze
kupata mikopo kutoka katika mfuko huo”.
Huu ni upendo wa ajabu kuwepo katika taifa letu uliofanywa na hayati Edward
Moringe Sokoine, ni tunu yenye kuinua maendeleo ya watu wengine.
Pengine naweza
kusema hawapo tena watu wenye mapenzi mema na taifa letu kama Sokoine, kama
wapo basi kunawalakini kwanini hawajitokezi? Watu twapaswa kufahamu kuwa umoja
wetu ndio utakao weza kutufanya tuyaenzi hayo kama tutamwamini Mungu wa kweli
aliye na huruma na pendo kwa watu aliowaumba. Tanzania tunakila sababu ya
kuendelea lakini kama tutakuwa na uzalendo na taifa letu, kwani mti wenye
matunda mazuri hauishi kupigwa mawe, tuchukue tahadhari katika kukwepa mawe
tutashinda uwezo tunao.
Historia
ya upendo wa mtu huanza toka katika familiya yake?.
Nakumbuka mimi
ningalimdogo mwenye umri wa miaka tisa, siku moja nilipokuwa naumwa, mama yangu
alinipeleka katika Hospital ya mtakatifu Francis Iliopo mjini Ifakara kutibiwa;
tulipoingia kwenye chumba cha daktari, yule daktari alimfukuza mama kwa kebei
kwamba hakuvaa mavazi mazuri, mama hakukubali kutoka kwasababu alikuwa
ananihurumia mwanae kwa kuwa nilikuwa naumwa sana, na kiukweli wazazi wangu
wote baba na mama walinipenda sana. Kiujumla sikukubaliana na maneno ya
daktari, nilimwambia mama twende nyumbani mimi ni mzima japo nilikuwa naumwa
sana, Kisha baba alinibeba mgongoni kama mtoto mchanga,hapo ulikuwa mhimili wa
kuwapenda wazazi wangu na kuwasikiliza kwa kila jambo. Niligundua wazazi wangu
walikubali aibu kwaajili yangu na ndugu zangu. Huo ulikuwa mwanzo wa upendo
hata kwa watu wengine wenye shida hasa wenye kipato duni na wasio na elimu.
Watu wengi
wakifanikiwa huwa wanaangukia kuwasahau wazazi wao na kuwadharau kana kwamba
hawakuzaliwa na kulelewa nao. Ninao mfano mzuri kwa baadhi ya watu wakotayari
kuwasaidia watu wengine ambao wanaowakubali na kupewa sifa kwamba wanahuruma na
busara lakini wazazi wao hawana chakula au mahitaji muhimu. Je huo ni upendo?
Au ni ushetani! Mungu wetu hakutuagiza hivyo bali amesema”Waheshimu Baba na mama yako ili
siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana Mungu wako”.(Kutoka
20:2-17))
Tuwe na upendo kwa
wazazi wetu, tukiwapenda tutawahurumia, na wala hatuta wasema vibaya au
kuwasema kwamba wanajidekeza, tukumbuke wote tunaelekea uzeeni na katika hali
walionayo, nawe utafikia, hakuna atakaye kwepa labda kwa mpango wa Mungu.
Lakini katika
imani ya Kikristo Biblia inatufundisha kwamba ni wajibu wa wazazi kuwaheshimu
na kuwatunza watoto wao katika misingi ya imani ya Kikristo, kama utakosa
kuwatunza katika imani uliyozaliwanayo utawajibika na maisha yake. Waefeso 6: 4 “Nanyi kina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na
mafundisho ya Bwana wetu Yesu Kristo.” Wazazi mkiwalea watoto wenu kwa
upendo na mshikamano nao watadumu katika mshikamano huo huo katika kuwakumbuka
siku za usoni pindi mkiishiwa nguvu za kujitafutia ninyi wenyewe katika hali ya
uzee. Mimi nawapenda wazazi wangu wewe je?......
“Ninawatakieni
ninyi ndugu amani, upendo na amani
kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.” Waefeso 6: 23
Mwisho nawashawishi
ndugu zangu tudumu katika pendo la kweli kama vile Mungu alivyo tupenda kwanza.
Waebrania 13: 1 “Upendo wa ndugu na uzidi kudumu msisahau kuwafadhiri wageni
No comments:
Post a Comment